mkutaano wa kuruhusu matumizi ya mbegu mpya unafanyika leo mjini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa hoteli ya New Safari iliyopo mjini hapa
watafiti kutoka katika vituo mbalimbalia vya kilimo hapa nchini wamekutana na wamekuja na aina mbalimbali za aina za mbegu,
akifungua mkutano huo kwa niaba ya wazirir wa kilimo chakula na ushirka Bwana Geofrey Kirenga aliwataka wadau wa mkutano huo kuchangagia mada kwa uhakika na umakini zaidi ili kuruhusu aina hizo mpya za mbegu ambazo ni .
HARAKATI
Wednesday, January 11, 2012
Monday, December 5, 2011
maafisa habari wakutana na kusherrehekea miaka 50 ya uhuru
hapa maafisa habari ambao walimaliza chuo kikuu cha waislam morogoro 9MUM) mwaka 2008 wakiwa wana adhimisha mika 50 ya uhuru na mika mitatu kazini katika uwanja wa Sabasaba mjini dsm
Sunday, December 4, 2011
MIAKA 50 YA UHURU
baadhi ya vyuo vikuu vya Tanzania vilivyosajiliwa kama tulivyolikuta bango katika banda la TCU katika maonesho ya mika 50 ya uhuru yanayoendelea kufanyika katika uwanja wa JK.Nyerere mjini DSM
Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika (kulia ) Bwana MbogoFutakamba akiwa na Mkurungenzi wa Usalama wa chakula Bwana emanuel Mtambo
Wataalam kutoka katika Kituo Cha utafiti cha Kibaha kinachohusika na utafiti wa Muhogo wakiwa wamebeba muhogo katika maonesho ya miaka 50 ya uhuru yaliofanyika katika viwanja vya sabasaba mjini DSM
Afisa masoko wa compuni ya uzalishaji wa mbegu ASA Bwana Kawamalakushoto katika banda la wizara ya kilimo chakula na ushirika
Mtaalam wa kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone Bwana Medad akiunganisha mabomba kwa ajili ya umwagiliaji wa mboga
afisa habari wa Rukwa bwana Hamza Temba katika harakati za kumpokea Raisi wa Zanziba Dr. Shein
Wednesday, November 2, 2011
mkutano wa Kazi kujadili mpango wa uwekezaji katika sekta ya Kilimo
Tanzania inategemea kuwa mwenyeji wa mkutano wa Kazi kujadili mpango wa uwekezaji katika sekta ya kilimo kwa muda wa siku mbili kuanzia tarehe 10 hadi 11 Novemba mwaka huu, hayo ni kwa mujibu wa Msimamizi wa Misaada ya Maendeleo na Uratibu wa Mashirikiano wa Kimataifa katika sekta ya kilimo kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Margaret Ndaba .
Ndaba amesema zaidi ya wajumbe 200 wanategemea kuhudhuria mkutano huo kutoka ndani na nje ya nchi ambao ni wadau wakubwa wa sekta ya kilimo.
Alizitaja tasisi zitakazoleta wajumbe wake kuwa ni wizara za sekta ya kilimo hapa nchini, wizara zinazofanyakazi na wizara za sekta za kilimo kama Wizara ya Miundo Mbinu, Fedha, Ardhi na Mandeleo ya Makazi, Makamu wa Rais na Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto.
Wizara nyingine alizitaja kuwa ni wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Mawasiliano na Uchukuzi, Elimu na Ufundi na wizara ya Sayansi na Teknolojia.
Pia wajumbe wa mkutano watatoka Sekta binafsi, Asasi zisizo za kiserikali, Muungano wa vyama vya Ushirika, Wabia wote waliosaini makubaliano ya kuendeleza sekta ya kilimo hapa Tanzania ( Tanzania CAADP Compact).
Wadau wakubwa wa kilimo ambao pia ni walengwa wa mkutano huu Wakulima, wataalikwa kupitia Muungano wa vikundi vya Wakulima (MVIWATA).
Tasisi zitakazo kuwa na wajumbe wake kutoka nje ya nchi kuwa ni pamoja na Umoja wa Africa ( AU), Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa (FAO) na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani la Umoja wa Mataifa (WFP).
Tasisi nyingine za nje zitakazoleta wajumbe wake katika mkutano huo kuwa ni pamoja na NEPAD, wawakilishi wa kanda za SADC, Jumuia ya Afrika mashariki na jumuia ya COMESA.
Washirika wa Maendeleo wa ndani na nje ya nchi pia wamealikwa katika mkutani huo, ambao aliwataja kuwa ni Shirika la Misaada Marekani (USAID), Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na Wawakilishi wa balozi za nje hapa nchini.
Alisema lengo kubwa la mkutano huo ni kujadili mpango mzima wa kuendeleza sekta za kilimo hapa nchini ili kuleta mapinduzi ya kweli katika kilimo kwa siku za usoni na hasa wakati huu wa utekelezaji wa azma ya Kilimo Kwanza.
Mada zitajikita zaidi kujadili mpango wa kuendeleza kilimo , utekelezaji wake na gharama husika ambapo serikali na wadau wake mbali mbali watahitajika kutoa matamko ya uchangiaji wa mpango huo, aliongeza Ndaba katika mazungumzo yake.
“Mkutano huo wa siku mbili utafanyika katika hoteli ya Hyatt Regency, Jijini Dar Es Salaam na wenyeviti wake watakuwa Mkamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dr Gharibu Bilali katika siku ya kwanza ya mkutano na siku ya pili ya kikao kitaendeshwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Jakaya Kikwete “ , alimalizia Ndaba.
Mlipuko wa panya
Kumetokea mlipuko wa panya hapa nchini katika wilaya zipatazo 8 na kuathiri kwa kiasi kukubwa uzalishaji wa mazao shambani na ghalani, kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Msaidizi wa Afya ya Mimea katika wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Dkt Fransisca Katagira.
Alizitaji wilaya zilizoathiriwa zaidi na mlipuko huo kuwa ni Bagamoyo na Kisarawe mkoani Pwani, Nanyumbu mkoa wa Mtwara na Lindi mkoni Mkoani Lindi.
Wilaya nyingine ni zilizopata athari za mlipuko huo wa panya waharibifu ni wilaya ya Morogoro, Kilosa, Mvomero na Ulanga zote za mkoa wa Morogoro, aliongeza Dkt Katagira.
Alifahamisha kuwa tayari kikosi kazi cha Wizara kimekwenda wilayani Bagamoyo chini ya Afisa Mfawidhi wa Kituo cha Kuthibiti Balaa la Panya kilichopo Morogoro Vctoria Ngowo ili kupambana na balaa hilo la mlipuko.
Taarifa za mlipuko wa panya kwa mara ya kwanza zilipokelewa kutoka wilaya ya Kilosa, kupitia Kituo cha Kuthibiti Balaa la Panya Agosti 8, 2011, alifafanua Dkt Katagira.
Dkt Katagira ameongeza kuwa panya hao wameshmbulia mbegu shambani zilizopandwa katika msimu wa vuli na kwenye maghala ya kuhifadhi mazao.
Monday, October 31, 2011
Subscribe to:
Posts (Atom)