Saturday, October 8, 2011

THAMANI YA ZAO LA KOROSHO IPO KWENYE MABIBO

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika hivi karibuni imekutana na  watafiti kutoka katika  kituo cha utafiti  cha  AMBRAPA kilichopo Brazil ili kufuatilia mradi wa kuongeza thamani ya zao la korosho baada ya kuvunwa Bibi Adelina  Aubert Ng'atigwa alisema kuwa mkutano huo umefanyika baada ya wizara kupeleka wataalam wanne katika kituo hicho nchini brazil kujifunza namna ya kuongeza thamani katika zao la koroshokupitia katika tunda la zao hilo (BIBO)

Aidha wataalam hao walisifia aina nzuri ya korosho inayolimwa nchini na kuwataka wakulima kulitumia tunda la korosho yaani bibo katika kuzalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo juice, keki, pipi  wisk na aina nyingi za mvinyo kama wanavyofanya kule brazili

hata hivyo wizara ipo katika mchakato wa makubaliano na kituo hicho ilikuweza kuwekeza hapa nchini na kuwa wakulima wetu elimu na mbinu mpya za uzalishaji wa zao hilo

No comments:

Post a Comment